Enrolment options
Moduli hii inatarajiwa kumfanya mwanafunzi afahamikiwe ujuzi wa jumla kuhusiana na fasihi linganishi kwa ajili ya lugha katika elimu. Wanafunzi watatambulishwa kwa masuala mengi mtambuka ya kinadharia, matini za kifasihi, kutalii masuala ya kihistoria na sasa yanayohusiana na usasa, usasaleo na utanadawazi. Hii itawasaidia wanafunzi kuchambua kazi mbalimbali za kifasihi kutoka katika visasili, dhamira na motifu za kiutu na zile za mikabala ya kifeministi zinazojitokeza kati sio tu katika tamaduni na nyakati tofauti bali pia zinajitokeza kwa waandishi tofauti pamoja na tanzu tofauti. Haya yote yatatazamwa mkazo ukiwekwa katika malengo ya ufundishaji wa lugha na fasihi katika elimu. Hii ikiwa na maana ya ufundishaji wa fasihi linganishi kwa minajili ya kufundishia lugha na fasihi katika elimu.